Dj Faster 80 Updates:
Home » , » wanafunzi wa shule ya msingi wajifunza TEHAMA kwa nadharia

wanafunzi wa shule ya msingi wajifunza TEHAMA kwa nadharia

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 22, 2013 | 1:15 PM



Shule ya msingi Gongoni  iliyopo manispaa ya Tabora bado inaendelea kujifunzia na kufundishia vifaa vya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA  kwa njia ya nadharia.

Kauli hiyo imetolewa leo na mwalimu mkuu wa shule ya msingi Gongoni bwana Khamisi Kibango wakati akizungumza na VOT FM STEREO ofisini kwake.

Amesema kuwa hivi karibuni serikali iliahidi kuleta vifaa vya kujifunzia na kufundishia vya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA  mashuleni ili kuongeza kiwango cha ufahamu na ufaulu kwa wanafunzi.

Mwalimu Kibango amefafanua kuwa tangu serikali ilipoahidi kuleta vifaa hivyo utekelezaji bado haujafanyika mashuleni hali inayowalazimu walimu kuendelea kufundisha kwa nadharia.

Aidha ameitaka serikali kupitia wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi imeombwa kutimiza ahadi iliyotoa ya kuleta vifaa vya kujifunzia na kufundishia vya teknolojia ya habari na mawasiliano TEHAMA  mashuleni.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii