Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Mbunge wa Tabora Kaskazini aitaka serikali kupitia upya madaraja ya tumbaku

Mbunge wa Tabora Kaskazini aitaka serikali kupitia upya madaraja ya tumbaku

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 29, 2013 | 7:17 PM



Serikali imesema inaanza kuyapitia upya madaraja ya zao la tumbaku ili kumnufaisha mkulima wa zao hilo.

Kauli hiyo ya serikali imefutia swali lililoulizwa leo Bungeni mjini Dodoma na mbunge wa jimbo la Tabora Kaskazini mheshimiwa Shaffin Sumar ambaye alitaka kujua ni lini serikali itayapunguza madaraja ya zao hilo yaliyopo sasa ambayo yanamnyonya mkulima.

Akitoa kauli ya serikali naibu waziri wa kilimo chakula na ushirika mheshimia Adam Malima amesema serikali kupitia bodi ya tumbaku TTB wameanza kuyapitia upya madaraja hayo zaidi ya sabini ili kuyashusha kufikia madaraja hamsini.

Katika swali lake la nyongeza mheshimiwa Sumar alisema madaraja ya tumbaku yanayotumika tanzania ni mengi ukilinganisha na nchi za Zambia na Zimbabwe na kwamba hayana tija kwa kuwa yanachangia kumnyonya mkulima wa zao hilo.

Aidha mbunge huyo ameitaka serikali kuchukua hatua dhidi ya ubadhilifu wa fedha za wakulima uliofanywa baina ya chama kikuu cha wakulima wa tumbaku kanda ya Magharibi WETCU na mabenki kupitia mikopo ya pembejeo na ujenzi wa maghala hali iliyosababisha wakulima kubebeshwa madeni wasiyostahili.

Akijibu hoja hiyo naibu waziri malima amebainisha kuwa serikali imeunda tume inayoongozwa na mkuu wa mkoa wa Tabora bibi Fatuma Mwasa kushughulikia na kwamba mapendekezo yatakayotolewa yatafanyiwa kazi na serikali.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii