Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Viongozi watakiwa kuzingatia misingi ya utawala bora

Viongozi watakiwa kuzingatia misingi ya utawala bora

Written By Voice of Tabora Radio on Friday, May 24, 2013 | 9:30 AM



Viongozi wa serikali za vijiji na kata wilayani Uyui wameshauriwa kuzingatia misingi ya utawala bora kwa kuwahudumia watu wenye ulemavu kama watu wengine.

Ushauri huo umetolewa  na mbunge wa Tabora kaskazini mheshimiwa Shafin Sumar wakati akizungumza na VOT FM STEREO kwa njia ya simu kutoka bungeni mjini Dodoma.

Amesema viongozi hao wakizingatia misingi ya utawala bora katika kutekeleza majukumu yao wataondoa changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha katika vikao vya maamuzi.

Mheshimiwa Sumar amebanisha kuwa endapo watu wenye ulemavu watashirikishwa kikamilifu katika vikao hivyo watapata fursa ya kuzisemea changamoto walizonazo na kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo.

Aidha amewataka watu wenye ulemavu wilayani humo kujiamini na kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuingia kwenye vikao vya maamuzi.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii