Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Chawata Uyui yapata viongozi wapya

Chawata Uyui yapata viongozi wapya

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 22, 2013 | 8:33 PM



Viongozi wa vyama vya watu wenye ulemavu wilayani Uyui wameaswa kuongoza  kwa kuzingatia uwazi na uwajibikaji ili kuepusha migogoro inayochangia kudhoofisha vyama hivyo.

Rai hiyo imetolewa  na mbunge wa jimbo la Tabora kaskazini mheshimiwa Shaffin Mamlo Sumar katika hotuba yake iliyosomwa na katibu wake bwana Said Katala wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama cha watu wenye ulemavu CHAWATA wilaya ya Uyui uliofanyika katika ukumbi wa kituo cha wanafunzi mjini hapa.

Mheshimiwa Shafin amesema viongozi hao wanapaswa kuwa chachu ya mabadiliko chanya kwa kuwaunganisha wanachama wao na kuzitumia rasilimali zilizopo kwa manufaa ya wote.

Aidha katika uchaguzi huo bwana John Kuka ametetea nafasi yake ya uenyekiti baada ya kushinda kwa kura saba dhidi ya mpinzani wake bwana Maganga Msabila aliyepata kura sita.

Viongozi wengine ni bwana Maganga Msabila amekuwa makamu mwenyekiti, bwana Husseni Gea amechaguliwa kuwa katibu na bibi Hindu Lupembelo amechaguliwa kuwa mtunza hazina wa chama hicho.

Mkutano huo umewachagua bwana Andrea Dotto kuwa naibu katibu na bwana Ally Said kuwa mtunza hazina msaidizi.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii