Dj Faster 80 Updates:
Home » » Serikali imewataka wakulima wa tumbaku kuuza tumbaku yao kwenye vyama vya msingi

Serikali imewataka wakulima wa tumbaku kuuza tumbaku yao kwenye vyama vya msingi

Written By Voice of Tabora Radio on Thursday, May 30, 2013 | 8:01 PM



Serikali mkoani Tabora imewataka wakulima za zao la tumbaku kuuza tumbaku yao kwenye vyama vyao vya msingi badala ya kuitorosha .

Mkuu wa mkoa wa Tabora bibi Fatuma Mwasa ametoa agizo hilo leo jioni wakati akikagua maandalizi ya soko la zao hilo litakalofanyika kesho katika ghala la kampuni ya TLTC lililopo Kiloleni mjini Tabora.
Amewataka wakulima wa zao hilo kuondoa hofu juu ya madeni wanayodaiwa kwani hakuna mkulima atakaye katwa fedha zake kabla ya madeni yake kuhakikiwa.

Bibi Fatuma amewaasa wakulima hao wa tumbaku kuuza tumbaku yao kwenye vyama vyao vya msingi ili kulinda haki zao kama wanachama wa vyama hivyo.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii