Dj Faster 80 Updates:
Home » » Mfuko wa Bima ya afya mkoa wa Tabora kutoa elimu kwa wanachama wake

Mfuko wa Bima ya afya mkoa wa Tabora kutoa elimu kwa wanachama wake

Written By Voice of Tabora Radio on Thursday, May 30, 2013 | 7:56 PM



Shirika la mfuko wa Bima ya afya limeanza kutoa elimu kwa wanachama wake katika Manispaa ya Tabora ili kuwapa uelewa wa kutambua wajibu wao katika chama hicho. 

Kauli hiyo imetolewa na kaimu meneja wa mfuko huo bwana  Godbless Mafole wakati wa mahojiano na VOT FM STEREO  kuhusu utoaji wa elimu kwa wanachama wao.

Amesema kuwa elimu hiyo itawasaidia wanachama kuwa na uelewa, kujua umuhimu na kutambua wajibu wao wanapoenda hospitali kupata matibabu.
Bwana Mafole ameelekeza kwamba wanachama wapokosa dawa hospitali wanatakiwa kwenda kwenye maduka ya famasi wakiwa na fomu za hospitali wanayopatia matibabu kwa ajili ya kupata dawa. 

Meneja  huyo amebainisha kuwa mfuko wa bima ya afya umesajili maduka manne katika mkoa wa Tabora pia unaendelea kusajili hadi vijijini ili kukidhi mahitaji ya dawa kwa wanachama wao. 

Aidha bwana Mafole ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Tabora kuwa kwa yeyote mwenye uwezo wa kufungua duka la   dawa lenye viwango vinavyokubaliwa  watalisajili  na mfuko huo.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii