Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Waislam mkoani Tabora watakiwa kukopa kwenye SACCOS ya kiislam

Waislam mkoani Tabora watakiwa kukopa kwenye SACCOS ya kiislam

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 29, 2013 | 8:48 PM



Waumini wa dini ya kiislam mkoani Tabora wameshauriwa kuchukua mikopo kwenye SACCOS za kiislamu kwa lengo maalum ili kujiinua kiuchumi kuanzia ngazi ya familia na taifa kwa ujumla.

ushauri huo umetolewa na mratibu wa SACCOS ya kiislamu mkoa wa Tabora Sheikh Said Mtungakoa wakati akizungumza na VOT FM STEREO ofisini kwake.

Ametahadharisha  kuwa baadhi ya waumini wa dini hiyo wamekuwa wakichukua mikopo pasipokuwa na malengo maalum na mwisho wanajikuta wanatumia fedha walizokopeshwa kwa matumizi mengine na kushindwa kufanya marejesho.

Mratibu huyo amefafanua kuwa unapohitaji kuwa mwanachama na kuchukua mkopo ni muhimu kujipanga kwa shughuli utakayofanya ili fedha utakayokopeshwa ijizalishe na kupata faida.

Aidha, Sheikh Mtungakoa amewataka waislam kuacha tabia ya manung’uniko ya kuwa wao hawawezeshwi kiuchumi na badala yake amewasihi wajiunge katika SACCOS za kiislam zisizokuwa na riba ili kujiendeleza na hatimae kujiinua kiuchumi.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii