Dj Faster 80 Updates:
Home » , , » Manispaa ya Tabora imetenga zaidi ya sh bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa barabara

Manispaa ya Tabora imetenga zaidi ya sh bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa barabara

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 29, 2013 | 8:18 PM

Picha kwa Hisani ya Mtandano-Maktaba


Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imepokea shilingi millioni  600 hadi sasa kutoka mfuko wa barabara  kwa ajili ya ujenzi wa barabara ikiwa jumla ya fedha zilizotengwa ni zaidi ya shilingi billioni moja nukta moja.
Kauli hiyo imetolewa  na mhandisi wa ujenzi wa barabara Manispaa ya Tabora bwana Edward Lemelo wakati wa mahojiano maalumu na VOT FM STEREO kuhusu utekelezaji wa ujenzi wa barabara za Manispaa hiyo.

Amezitaja barabara ambazo zimekamilika hadi sasa kuwa ni barabara ya Kisarika yenye urefu wa kilometa 24 nukta 46, barabara ya Soweto yenye kilometa  0.67, barabara ya Mwinyi yenye kilometa 2 nukta 1 na barabara Ndevelwa yenye urefu wa kilometa  19 nukta 85.

Amesema ujenzi wa barabara ulianza  mwaka jana  ukiwa umegawanyika katika makundi makuu mawili ya  matengezo ya kawaida na matengenezo makubwa unaotarajiwa kumalizika Juni 30 mwaka huu.

Aidha bwana Edward amesema halmashauri ya Manispaa ya Tabora katika mwaka huu wa fedha imetenga fedha kwa ajili ya kuweka lami barabara ya Lumaliza - Mwanza  yenye kilometa mbili ikiwa ni utaratibu wa kila mwaka.

Mhandisi huyo amebainisha kuwa wamekarabati greda la kuchonga barabara ambazo hazipo kwenye orodha na zoezi hilo litaanza muda wowote kwa kila kata.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii