Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Manispaa ya Tabora inaupungufu wa wauguzi katika zahanati na vituo vya afya

Manispaa ya Tabora inaupungufu wa wauguzi katika zahanati na vituo vya afya

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 22, 2013 | 1:18 PM



Asilimia 40 ya wauguzi wanahitajika katika kata za manispaa ya Tabora ili kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye vituo vya afya.

Kauli hiyo imetolewa na afisa muuguzi wa manispaa ya Tabora bibi Devota Msele wakati akizungumzia changamoto mbalimbali  zinazowakabili katika uwajibikaji.

Amesema wauguzi hao wanaohitajika ni kwa ajili ya vituo vya afya wilayani Tabora ili kupunguza msongamano wa wagonjwa wakati wa kutibiwa.

Bibi Devota ameitaja changamoto nyingine kuwa ni upungufu wa vifaa tiba zikiwemo dawa hali ambayo huwalazimu baadhi ya wagonjwa kununua dawa walizoandikiwa kwenye maduka ambazo hazipo hospitali.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii