Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Viongozi wa dini mkoani Tabora waombwa kuhamasisha uchangiaji wa damu

Viongozi wa dini mkoani Tabora waombwa kuhamasisha uchangiaji wa damu

Written By Voice of Tabora Radio on Wednesday, May 29, 2013 | 7:27 PM



Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini mkoani Tabora wameshauriwa kuwa na ushirikiano katika kuhamasisha waumini wao kuhusu uchangiaji damu.

Ushauri huo umetolewa leo na afisa mhamasishaji wa Mpango wa taifa wa damu salama kanda ya Magharibi bwana Costantine Thadeo wakati akizungumza na VOT FM STEREO.

Amesema kuwa viongozi hao wanatakiwa kuwahamasisha waumini kuhusu uchangiaji damu ili kuweza kufikia malengo waliojiwekea kupitia mpango huo wa taifa wa damu salama.

Afisa huyo wa mpango wa taifa wa damu salama kanda ya Magharibi amesema katika kipindi cha maadhimisho ya siku ya uchangiaji damu kwa mwaka huu wanatarajia kukusanya chupa  zaidi ya 1,500.

Bwana Thadeo amefafanua kuwa malengo mengine waliojiwekea ni pamoja na kuendelea kuhamasisha jamii kuchangia damu, kutoa elimu kwa viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini na kwa jamii kupitia vyombo vya habari na mikutano ya hadhara.  

Aidha maadhimisho hayo ya uchangiaji damu duniani hufanyika juni 14 kila mwaka ambapo kwa mwaka huu kitaifa yatafanyika mkoani mara na kwamba yamebeba ujumbe wa kauli mbiu isemayo changia damu ni zawadi ya maisha.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii