Dj Faster 80 Updates:
Home » , » Miradi ya umeme vijijini kukamilika Septemba mwaka huu

Miradi ya umeme vijijini kukamilika Septemba mwaka huu

Written By Voice of Tabora Radio on Monday, May 20, 2013 | 10:36 PM



Serikali imesema kuwa miradi ya usambazaji wa huduma ya umeme vijijini unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.

Waziri wa nishati na madini mheshimiwa Sospeter Muhungo ametoa kauli hiyo  Bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Busanda mheshimiwa Lolensia Bukwimba aliyetaka kufahamu ni lini miradi hiyo ya usambazaji wa nishati ya umeme vijijini itakamilika.

Mheshimiwa Muhongo amefafanua kuwa kulingana na wafadhili wa miradi hiyo ambao ni serikali ya Marekani miradi hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Septemba mwaka huu.

Aidha utekelezaji wa miradi hiyo ndani yake kuna miradi midogo arobaini na moja ya usambazaji wa umeme kwenye mikoa kumi na sita ya tanzania bara miongoni mwa mikoa hiyo ni Tabora, Arusha, Kilimanjaro, Manyara, na Tanga.

mikoa mingine ni  Pwani, Morogoro, Dodoma, Singida, Mbeya, Rukwa, Kigoma, Kagera, Mwanza, Mara pamoja na Shinyanga.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Listen Live VOT FM.High quality

Total Visit


TELECENTRE

Michezo Videos

 
Powered by Blogger | © Voice of Tabora Radio 89.0Mhz - All Rights Reserved
Developed by Kicbjamii